Kimbunga Hellen chaua 59 na kusababisha maafa Marekani

 

Mvua kubwa inayoambatana na kimbunga Helene imeleta madhara katika maeneo ya  North Carolina na Tennessee kusini mashariki mwa Marekani na kusababisha vifo vya watu 59.

Mji wa mlimani wa Asheville uliopo North Carolina umetenganishwa na mafuriko katika siku ya Jumamosi.

Watu zaidi ya 400 wamelazimika kutotoka nje katika jimbo hilo, ambalo watu 10 wamekufa. Mahitaji ya kila siku yamelazimika kupelekwa kwa njia ya anga, amesema Gavana wa jimbo hilo Roy Cooper.

Maafisa wameendelea kufanya uokoaji kwa kutumia boti, helkopta na magari makuwa kusaidia watu waliokwama kwenye mafuriko.

Wafanyakazi wapatao 50 na wagonjwa wao wamelazimika kujikusanya juu ya paa la jengo la hospitali ya Tennesse.

Chapisha Maoni

0 Maoni