Amani ni hakika wa usalama wa wanawake na watoto na huboresha ustawi wa familia

 

Katika jamii ya Tanzania, wanawake na watoto ndio wanaoumia zaidi pale amani na utulivu wa nchi unapovurugika. Maoni kutoka mkoani Simiyu yanaonesha kuwa jamii inathamini amani kuliko siasa.

Spora Ngh’wani, mkazi wa Bariadi, anaelezea hofu yake: "Amani na utulivu ni muhimu sana katika jamii, nchi na hata familia. Sisi wanawake ndiyo tegemeo kubwa kwa familia zetu, ndiyo wajasiriamali, walezi wa familia pia. Amani ikitoweka, watu wa kwanza kupata shida ni sisi wanawake na watoto wetu. Sisi tunapenda amani kuliko vitu vyote."

Kauli hii inaungwa mkono na Rebeca Shilinde wa Busega, anayesisitiza athari za kisaikolojia: "Kama binadamu ukikosa amani na utulivu hata moyoni mwako huwezi kufanya kazi yoyote ile, kila wakati utabaki na wasiwasi mkubwa. Hivyohivyo nchi ikikosa amani na utulivu hakuna jambo litafanyika. Kila Mtanzania anayo sababu ya kuilinda hii amani."

Ustawi wa jamii unategemea amani. Ukosefu wa amani unavuruga elimu ya watoto, unazuia upatikanaji wa huduma za afya, na unaleta hofu isiyo na msingi kwa wazazi.

Ujumbe mkuu unaotolewa na sauti hizi ni kwamba hakuna malengo ya kisiasa yanayoweza kuhalalisha kuvuruga ustawi na amani ya familia. Maandamano ya vurugu ni chanzo cha hofu, na wananchi wanashauriwa kukataa miito yote inayohatarisha maisha yao na ya vizazi vyao.

Chapisha Maoni

0 Maoni