MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Jumuiya za Ukanda wa Maziwa Makuu na Nchi Wanachama wa Mkataba wa Amani, Usalama na Ushirikiano kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Eneo la Maziwa Makuu, uliyofanyika Ikulu ya Entebbe nchini Uganda.
Mkutano huo, umejadili
hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika
kutafuta amani ya kudumu ya eneo hilo.
Katika Mkutano huo, Makamu
wa Rais ameambatana na Waziri Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais (Sera,
Uratibu na Baraza la Wawakilishi) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hamza
Hassan Juma pamoja na Naibu Waziri wa Mambo Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki Dkt. Ngwaru Maghembe pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Uganda Mhe.
Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli.


0 Maoni