Wataalamu wa afya wameshauri
kuchukuliwa kwa hatua za haraka na madhubuti ili kupunguza kiwango cha uchafuzi
wa hewa, huku wakisisitiza umuhimu wa sera za mazingira zinazolenga kulinda
afya ya wananchi hasa watoto.
Wataalamu wameonya
kuwa uchafuzi wa hewa umefikia viwango vya hatari na sasa unatishia siyo tu
afya ya mapafu bali pia unasababisha kiharusi, magonjwa ya moyo, matatizo ya
akili ya kusahau (dementia), wasiwasi na msongo wa mawazo (depression).
Kwa mujibu wa taarifa
za Shirika la Afya Duniani (WHO), watu tisa kati ya kumi duniani wanapumua hewa
chafu isiyokidhi viwango salama vya kiafya. Uchafuzi huo unajumuisha chembe
chembe ndogo ambazo zinaweza kuingia ndani kabisa ya mapafu na hata kufikia
ubongo wa binadamu.
0 Maoni