Waziri wa Katiba na
Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, ameitaka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS) kuongeza
umakini katika kutekeleza majukumu yake kabla, wakati na baada ya Uchaguzi
Mkuu, akisisitiza kuwa sheria haziendi likizo kipindi cha uchaguzi.
Akizungumza wakati wa
hafla ya kukabidhi magari 16 kwa ofisi za mashtaka za wilaya 16, Dkt. Ndumbaro
amesema uzoefu unaonyesha kuwa katika kipindi cha uchaguzi baadhi ya watu
hufanya vitendo vinavyotishia amani, jinai, kashfa na udhalilishaji wakiamini
sheria hazifanyi kazi.
Waziri Dkt. Ndumbaro
ameongeza kwa kutaka kila anayekiuka sheria achukuliwe hatua bila kujali nafasi
yake, “Machafuko mengi yanatokea kipindi cha uchaguzi, msimfumbie macho watu
wanaovunja sheria.”
0 Maoni