Mwana wa Mfalme Kutoka Afrika Kusini Avutiwa na Fursa za Misitu na Utalii Sabasaba

Wageni mbalimbali wanaendelea kumiminika kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba wakijionea fursa zinazotolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii, hususan kwenye sekta ya misitu na utalii wa ikolojia.

Miongoni mwa wageni hao ni Mwana wa Mfalme Celipilo Ngobese kutoka Kwazulu Natal, Afrika Kusini, ambaye leo Julai 11, 2025 ametembelea banda la Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Ngobese alipata fursa ya kuona shughuli za ufugaji nyuki, uhifadhi wa misitu na vivutio vya utalii wa ikolojia vinavyosimamiwa na TFS, akieleza kuvutiwa na jitihada za Tanzania katika kuhifadhi rasilimali za misitu na kuzitumia kwa maendeleo endelevu.

Maonesho ya SabaSaba yanaendelea Jijini Dar es Salaam yakihusisha taasisi mbalimbali za serikali na sekta binafsi, huku yakilenga kuvutia wawekezaji na wadau wa ndani na nje ya nchi.



Chapisha Maoni

0 Maoni