Muhimbili yashiriki NBC Dodoma Marathon 2025

 

Watumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Upanga na Mloganzila, leo Julai 27, 2025 wameshiriki mbio za zilizoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara, NBC Dodoma Marathon 2025 kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kuboresha huduma za afya, hususan afya ya mama na mtoto pamoja na kuhamasisha umuhimu wa mazoezi kwa afya bora.

Akizungumza mara baada ya kumaliza mbio hizo, Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji MNH-Upanga Dkt. Rachel Mhavile, amesema ushiriki wao ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za NBC katika kuboresha huduma za afya nchini, hususan kwa mama na mtoto.

Dkt. Mhavile ameongeza kuwa mazoezi ni muhimu kwa watumishi wa afya na jamii kwa ujumla, kwani husaidia kuweka miili katika hali bora ya afya na kujikinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.

Chapisha Maoni

0 Maoni