Mhe. Majaliwa awasili Beralus kuanza ziara ya kikazi

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana Julai 21, 2025 amewasili nchini Belarus kuanza ziara ya kikazi nchini humo.  Kwenye  Uwanja wa Ndege wa Kinsk alipokelewa na Naibu Waziri Mkuu wa Beralus,  Viktor Karankevich.

Katika ziara hiyo siku ya Kwanza Mheshimiwa Waziri Mkuu ataweka shada la maua katika mnara wa mashujaa wa Jamhuri ya Beralus.

Pia atatembelea kiwanda cha kutengeneza Matrekta na vifaa mbalimbali  vya kilimo (Minsk Tractor Plant) na baadae atakutana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Belarus Mhe. Alexander Turchin.

Katika ziara hiyo ameambatana na Balozi wa  Tanzania Urusi na Belarusi, Frederick Ibrahim Kibuta ,  Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Kazi , Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Shariff Ali Shariff na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Cosato Chumi.



Chapisha Maoni

0 Maoni