Mafuriko yaua watu 24, wasichana wengi hawajulikani walipo Texas

 

Operesheni kubwa ya uokoaji na utafutaji watu imeendelea usiku kucha huko Texas nchini Marekani baada ya mafuriko ya ghafla kusababisha vifo vya watu wasiopungua 24 na kutoonekana kwa  wasichana wengi waliokuwa kwenye kambi ya majira ya joto ya Kikristo.

Kulikuwa na onyo dogo kabla ya Mto Guadalupe kujaa kwa futi 26 (sawa na mita 7.9) kwa muda wa chini ya saa moja, na mafuriko yaliyofuata yalisomba nyumba kuhamishika, magari, na vibanda vya mapumziko ambako watu walikuwa wakisherehekea wikendi ya tarehe 4 Julai.

Vikosi vya uokoaji bado vinaendelea kuwatafuta hadi watoto 25 waliokuwa miongoni mwa wasichana 750 waliokuwa wakihudhuria Kambi ya Mystic, iliyoko nje kidogo ya mji wa Kerrville, kilomita 104 kaskazini-magharibi mwa San Antonio.

Hali ya hatari imetangazwa katika wilaya kadhaa ambapo barabara nyingi zimesombwa na maji na mawasiliano ya simu yamekatika.

Rais wa Marekani Donald Trump ameita tukio hilo "la kushtua" na "la kutisha," huku ya Marekani  White House ikiahidi msaada wa ziada.

Picha zinaonyesha maji mengi ya mafuriko yamejaa hadi juu ya madaraja na maji yanayotiririka kwa kasi yakipita barabarani.



Chapisha Maoni

0 Maoni