Bilionea Elon Musk kuanzisha chama kipya Marekani

 

Bilionea Elon Musk amesema kwamba anazindua chama kipya cha kisiasa nchini Marekani, ikiwa ni wiki chache tu baada ya kutofautiana vikali na Rais wa Marekani, Donald Trump.

Tajiri huyo ametangaza kupitia jukwaa lake la kijamii, X, kwamba ameanzisha chama kipya kinachoitwa America Party, kitakachotoa changamoto kwa mfumo wa vyama viwili vya Republican na Democratic.

Hata hivyo, haijajulikana kama chama hicho tayari kimesajiliwa rasmi na mamlaka za uchaguzi za Marekani. Musk, alizaliwa nje ya Marekani na hivyo hastahili kugombea urais wa Marekani, hajasema ni nani atakayekiongoza chama hicho.

Musk alianza kuzungumzia uwezekano wa kuanzisha chama hicho wakati wa ugomvi wake wa wazi na Rais Trump, ambao ulimfanya ajiuzulu kutoka kwenye nafasi yake katika utawala huo na kuingia kwenye mzozo mkali wa hadharani na mshirika wake wa zamani.



Chapisha Maoni

0 Maoni