Bilionea Elon Musk
amesema kwamba anazindua chama kipya cha kisiasa nchini Marekani, ikiwa ni wiki
chache tu baada ya kutofautiana vikali na Rais wa Marekani, Donald Trump.
Tajiri huyo
ametangaza kupitia jukwaa lake la kijamii, X, kwamba ameanzisha chama kipya
kinachoitwa America Party, kitakachotoa changamoto kwa mfumo wa vyama viwili
vya Republican na Democratic.
Hata hivyo,
haijajulikana kama chama hicho tayari kimesajiliwa rasmi na mamlaka za uchaguzi
za Marekani. Musk, alizaliwa nje ya Marekani na hivyo hastahili kugombea urais
wa Marekani, hajasema ni nani atakayekiongoza chama hicho.
Musk alianza
kuzungumzia uwezekano wa kuanzisha chama hicho wakati wa ugomvi wake wa wazi na
Rais Trump, ambao ulimfanya ajiuzulu kutoka kwenye nafasi yake katika utawala
huo na kuingia kwenye mzozo mkali wa hadharani na mshirika wake wa zamani.
0 Maoni