Waziri Mkuu wa India, Modi atembelea eneo la ajali ya ndege ya Air India

 

Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, ametembelea eneo la ajali ya ndege ya Air India iliyotokea Alhamisi, ambapo watu wote isipokuwa mmoja kati ya 242 waliokuwa ndani ya ndege hiyo waliaga dunia. 

Ndege hiyo ilikuwa ikielekea London kabla ya kuanguka kwenye eneo la makazi muda mfupi baada ya kupaa. 

Hadi sasa haijafahamika ni watu wangapi waliopoteza maisha ardhini, ingawa afisa mmoja ameiambia BBC kwamba watu wasiopungua wanane wamefariki dunia kutokana na ajali hiyo. 

Mtu pekee aliyeokoka ni raia wa Uingereza, Vishwashkumar Ramesh, aliyekuwa ameketi kwenye kiti namba 11A, anaendelea kupata matibabu hospitalini. Kaka yake amesema "hatambui namna alivyonusurika ajali." 

Kwa mujibu wa shirika la ndege la Air India, abiria waliokuwemo walijumuisha raia 169 wa India, 53 wa Uingereza, saba wa Ureno na mmoja wa Canada. 

Familia za waliopoteza maisha zimeanza kutoa sampuli za vinasaba (DNA) kusaidia katika utambuzi wa miili ya wapendwa wao.

Chapisha Maoni

0 Maoni