Watanzania 42 waliokwama Israel kurejea leo nchini

 

Watanzania 42 waliokwama nchini Israel kufuatia mapigano kati ya nchi hiyo na Iran, wanatarajiwa kurejea nchini leo, Juni 25, 2025 kwa kutumia ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia (Ethiopian Airlines).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Serikali, kurejea kwa Watanzania hao ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, aliyelitaka Serikali kuhakikisha wananchi wake waliokwama nje ya nchi kutokana na hali ya machafuko, wanarejea nyumbani wakiwa salama.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Watanzania hao watawasili nchini kwa makundi mawili. Kundi la kwanza limewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Unguja saa 6:55 mchana, huku kundi la pili likitarajiwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam saa 11:55 jioni.



Chapisha Maoni

0 Maoni