Rais Mwinyi ashiriki sala ya Eid Al Adha

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi amejumuika pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Eid Al Adha iliyosaliwa Masjid Taqwa, Wilaya ya Kati,  Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar leo tarehe 7 Juni 2025.

Mapema baada ya sala hiyo, Rais Dkt. Mwinyi alifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja kuchinja mnyama(Udh-hiya) ikiwa ni sehemu ya Ibada  na kutoa mkono wa Eid kwa Masheikh wa Mkoa huo.



Chapisha Maoni

0 Maoni