Balozi wa China atembelea Hifadhi ya Dunia Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songomnara

 

Balozi wa China Nchini, Chen Mingjian ametembelea Hifadhi ya Urithi wa Dunia Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songomnara jana Juni 24,2025.

Katika safari yake alipata kujionea vivutio vya utalii vilivyopo katika Magofu ya Kilwa Kisiwani na kupata maelezo kuhusu historia ya Biashara kati ya Kilwa Kisiwani na China mnamo karne ya 13 kutoka kwa wahifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania.

Balozi Chen Mingjian aliambatana na watalii wengine 10 kutoka Nchini China pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe.Mohamed Nyundo.




Chapisha Maoni

0 Maoni