Mkuu wa Mkoa wa Dodoma azindua rasmi Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani

 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amezindua rasmi leo hii maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani na kuwasihi wadau wa sekta ya nyuki na misitu pamoja na utalii kutembelea mabanda yaliyoko katika maonesho ili kupata elimu na maarifa kutoka kwa wadau wa sekta ya Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Ufugaji wa Nyuki.

Maadhimisho hayo yaliyozinduliwa leo hii yanafanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma kuanzia Mei 17 hadi 20, 2025 yakiongozwa na kauli mbiu isemayo "Nyuki kwa Uhai na Uchumi Imara, Tuwahifadhi" Apimondia 2027 Tanzania Ipo Tayari.

Mhe. Senyamule amesema kauli mbiu hii inawakumbusha Watanzania kuhusu mchango wa Nyuk katika afya zetu kutokaka na matumizi ya mazao mengi anayozalisha kama vile chavua, sumu pamoja na maziwa ikiwa ni pamoja na kujipatia kipato kupitia mazao hayo.

Aidha amefurahishwa na biadhaa mbalimbali zilizotenengezwa na wafanyabiashara na wajasiriamali ikiwamo zile zitokanazo na mazao ya nyuki wakati akifanya ziara yake katika mabanda ya maonesho akisema ni kielelezo kuwa bidhaa zitokanazo na Nyuki ni tiba kwa matumizi mballimbli ya afya lakini pia ni sehemu ya kupata kipato na kujiiunua kiuchumi.

“Nimeona watu wakiuza asali ambapo watu wanapata kipato na wakuwa kiuchumi, nimeona watu wakitengeneza mazao mbali mbali ya Nyuki,” alisema.

Pamoja na hayo amesema kuwa maonesho haya yatafungwa rasmi na Mhe. Kassima Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kama mgeni rasmi huku akitoa wito kwa wananchi wote wa mkoa wa Dodoma kuungana na Waziri Mkuu katika kufunga maonesho hayo.




Chapisha Maoni

0 Maoni