Rais Samia atua nchini na kwenda kwenye ajali ya jengo K’koo

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema hadi kufikia asubuhi ya leo tarehe 20/11/2024 watu 20 wamefariki kutokana na maafa ya ghorofa lililoporomoka Kariakoo, Dar es Salaam.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo alipofika katika eneo la tukio hilo Kariakoo, ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kurejea kutoka nchini Brazil, ambapo amekagua shughuli za uokoaji na kisha kuongea na wananchi.

 “Jitihada zetu kubwa katika tukio hili imekuwa kuwaokoa wenzetu walionasa katika jengo hili wakiwa hai lakini kama tunavyoambiwa jitihada haziondoshi kudra ya Mungu, pamoja na jitihada tulizofanya kuna wenzetu tumewapoteza,” alisema Rais Samia kwa huzuni.

 “Hili sio pigo kwa familia zilizopoteza eatu wao pekee yao ni pigo letu kama Watanzania na tunaguswa pia, ni kumbukumbu ya kutisha kwa wenzetu waliookoka hapa, kwa jinsi jengo lilivyo mtu akitoka hai bila shaka hawapo sawa kisaikolojia, niombe wasifadhaike, wajipe moyo na tuendelee na shughuli zetu za kawaida bado Mungu ana kazi nao.”


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua eneo la maafa ya ajali ya kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Novemba, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua eneo la maafa ya ajali ya kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Novemba, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwajulia hali na kuwapa pole majeruhi wa ajali ya kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo ambao wamelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Novemba, 2024.

Chapisha Maoni

0 Maoni