Vijana 2,100 wakiwemo 32 wa kutoka
Musoma Vijijini, wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) walianza
matembezi ya miguu kutokea Butiama hadi Mwanza siku ya Jumatano, 9.10.2024.
Matembezi haya yanafuata nyayo za
matembezi ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
aliyoyafanya Mwaka 1967 akiunga mkono Azimio la Arusha lililozaliwa mwaka huo
(1967).
Vilevile, matembezi haya ni sehemu ya
sherehe za kilele cha ukimbizaji Mwenge wa Uhuru zitakazohitimishwa Jijini
Mwanza tarehe 14.10.2024
0 Maoni