Vijana wa UVCCM watembea kutoka Butiama hadi Mwanza

 

Vijana 2,100 wakiwemo 32 wa kutoka Musoma Vijijini, wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) walianza matembezi ya miguu kutokea Butiama hadi Mwanza siku ya Jumatano, 9.10.2024.

Matembezi haya yanafuata nyayo za matembezi ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoyafanya Mwaka 1967 akiunga mkono Azimio la Arusha lililozaliwa mwaka huo (1967).

Vilevile, matembezi haya ni sehemu ya sherehe za kilele cha ukimbizaji Mwenge wa Uhuru zitakazohitimishwa Jijini Mwanza tarehe 14.10.2024

Chapisha Maoni

0 Maoni