Madereva wa mashindano ya magari wameeleza kuridhishwa kwao na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa kutoa maeneo bora ya kufanya mashindano, ambayo yameimarisha ushindani katika mchezo huo.
Pongezi hizo zilitolewa jana wakati wa
mashindano ya magari yaliyofanyika katika shamba la miti lililoko Morogoro,
wilayani Mvomero, yakiwa na ushiriki wa magari 17, yaliyoandaliwa na Klabu ya
Milima ya Uluguru.
Kaimu Kamanda wa Kanda ya Mashariki,
PCO Mathew Ntalicha, amewataka waandaji wa mashindano kuendelea kutumia maeneo
yaliyo chini ya TFS. Alisisitiza kuwa hii itasaidia kueneza elimu kuhusu
uhifadhi wa mazingira kwa jamii.
Mashindano haya ni fursa muhimu ya
kukuza michezo na kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa misitu.
0 Maoni