Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Dkt. Pindi Chana (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Kenya nchini
Tanzania, Mhe. Isaac Njenga pembezoni mwa Onesho la Kimataifa la Swahili
International Tourisim Expo-S!TE (S!TE 2024) jijini Dar es Salaam.
Lengo la kikao hicho kilichofanyika
jana ni kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano katika Sekta ya Maliasili
na Utalii baina ya nchi za Kenya na Tanzania.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dunstan Kitandula, Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Dkt. Ramadhan Dau, Naibu Katibu
Mkuu anayeshughulikia Utalii, Nkuba Mabula, Mkurugenzi Mkuu Bodi za Utalii
Tanzania(TTB), Ephraim Mafuru na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Dkt. Thereza
Mugobi.
0 Maoni