Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili
na Utalii anayeshughulikia Uhifadhi,
Kamishna wa Polisi (CP), Benedict Wakulyamba, amesema Jeshi la Polisi
litaendelea kutoa elimu na mafunzo kwa Jeshi la Uhifadhi nchini ili liweze
kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia misingi ya sheria, kanuni,
miongozo na taratibu zilizoanzisha jeshi hilo.
CP. Wakulyamba ameyasema hayo jana 22,
2024 alipotembelea Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Saanane na kuteta na maafisa na
askari kutoka TANAPA, TAWA na TFS ndani ya ukumbi wa Taasisi ya Taaluma ya
Wanyamapori Pasiansi jijini Mwanza.
Akiongozana na Warakibu wawili kutoka
Makao Makuu ya Polisi jijini Dodoma CP. Wakulyamba alisema, "Jeshi la
Polisi litashirikiana nanyi kutoa elimu
na mafunzo mbalimbali hususani juu ya kufuata kanuni za Haki Jinai
zinazohusisha ukamataji salama, kuheshimu
haki za binadamu na kutii sheria za upekuzi na kuhodhi mali za uhalifu.”
Aidha, amewataka maafisa na askari wa
Jeshi la Uhifadhi kuendelea kuimarisha
ulinzi na kusimamia Maliasili zilizopo kwani Taifa lina imani kubwa sana kwenu
ndo maana mmepewa dhamana hiyo.
Katika ziara hiyo, CP Wakulyamba,
licha ya kutoa mafunzo, pia ametembelea na kuteta na askari wa Lamai na
Kenyanganga ndani ya Hifadhi ya Taifa Serengeti wilaya ya Tarime Mkoani Mara.
Na. Brigitha Kimario- Mwanza
0 Maoni