Mwanamke mmoja wa Mkazi wa Matalawe
Mjini Njombe, Joyce Ojala (32), anashikiliwa na polisi kwa kosa la kutoa taarifa
za uongo kuwa ametekwa na watu wasiojulikana ili kumlazimisha mumewe Mfaume
Hussein Mzee (37), aliyekuwa Mkoani Ruvuma kwa zaidi ya miezi sita akifanya
kazi za madini kurejea nyumbani.
Akisimulia tukio hilo Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Njombe, Mahamoud Banga, amesema Joyce alitoa taarifa kwa mumewe
akidai ametekwa na kwamba mume wake anatakiwa kurudi haraka ili kushughulikia
suala hilo.
Amesema baada ya Mfaume, kupokea
taarifa hiyo na kuamua kurejea mara moja nyumbani baada ya kuambiwa kuwa mkewe
yuko hatarini lakini alipofuatilia polisi ilibainika kuwa hakuna tukio la
utekaji na kwamba mwanamke huyo alijiteka mwenyewe kutokana na wivu wa mapenzi.
Kamanda Banga ameeleza kuwa mume huyo
alikuwa akiwasiliana na mke wake mara kwa mara na kumjulisha kuwa anafanya
shughuli za madini na hana uwezo wa kurudi mara moja hata hivyo mwanamke huyo
aliingia wivu na kuamua kutengeneza kisa hicho cha utekaji ili kumfanya mume
wake kurudi.
0 Maoni