Mwanamke mmoja nchini Australia
anapigania uhai wake hospitali baada ya kung’atwa mkono na mbwa wake na kuukata
kaskazini mwa Queensland.
Vikosi vya uokoaji vililazimika kuitwa
kuokoa maisha ya mwanamke huyo katika mji wa pwani wa Twonville, na kumkuta
akiwa katika hali mbaya.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 34,
mkono wake wa kulia ulikuwa na majeraha makubwa na kukatika kwenye sehemu ya
kiwiko.
Polisi walilazimika kumpiga risasi na
kumuua mbwa huyo aina ya pit bull ambaye alikuwa amefungiwa ndani ya nyumba
huku akiwa na hasira kali.
Polisi wamesema walipowasili walimkuta
mwanamke huyo akitokwa damu nje ya nyumba na mbwa wake akiwa ndani huku akihaha
kutoka nje kwa hasira.
0 Maoni