Mamilioni ya watu waliopo Florida
nchini Marekani wanaharakisha kuondoka kwenye nyumba zao, wakati kimbunga
Milton kikielekea kulikumba jimbo hilo la pwani ya mashariki.
Kimbunga Milton chenye ukubwa wa daraja
la tano, kinatarajiwa kulikumba eneo la Tampa usiku, kikiambatana na upepo
mkali wenye kasi ya kilomita 270 kwa saa.
Rais wa Marekani Joe Biden ameonya na
kusema kuwa kuondoka ni suala la “uhai na kifo”, wakati jimbo hilo likifanya
jitihada za kuhamisha idadi kubwa ya watu kuwahi kutokea katika miaka ya hivi
karibuni.
0 Maoni