Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mheshimiwa Said mshana amekutana na kuzungumza na Waziri wa Michezo na Burudani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Didier Budimbu Ntubuanga.
Kikao hicho kimefanyika Ofisini kwa
Mhe. Waziri Ntubuanga jijini Kinshasa
Mhe. Balozi alikwenda kuonana na Mhe.
Waziri kwa ajili ya kumshukuru kwa mapokezi mazuri ambayo Serikali ya DRC
imeipatia timu ya Taifa ya Tanzania iliyoko nchini DRC kwa ajili ya mchezo wake
na timu ya Taifa ya DRC unaotarajiwa kufanyika tarehe 10 Oktoba 2024 jijini
Kinshansa nchini DRC.
Taifa Stars inakutana na Timu ya Taifa
ya DRC maarufu kwa jina la Chui, kwa ajili ya mchezo wa kufuzu fainali za
Mataifa ya Afrika zinazotarajiwa kufanyika nchini Morroco mwaka 2025.
0 Maoni