Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila imepokea msaada wa
vifaa tiba kutoka Taasisi ya Afya Ifakara (IHI) chini ya mradi wa NEST 360
ambao una lengo kuboresha huduma kwa watoto wachanga wanaohudumiwa kwenye
kitengo cha uangalizi maalum kwa watoto wachanga chini ya siku 28.
Msaada uliotolewa ni pamoja na mashine za tiba mwanga
(phototherapy machines), mashine za kufuatilia joto kwa watoto wachanga na
vifaa tiba vingine ambavyo vinatumika kutoa huduma katika kitengo hicho ambavyo
jumla yake vina gharama ya takribani TZS 53 Mil.
Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji MNH,
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Tiba Shirikishi. Dkt. Lulu Sakafu ameishukuru
taasisi hiyo kwa msaada huo na kuongeza kuwa vitasaidia kuboresha huduma za
watoto na hivyo wameienzi falsafa ya huduma bora kwa mteja kwa vitendo.
"Tunawashuru (NEST360) kwa kutambua umuhimu wa watoto
wachanga kwakuwa wao ni taifa la kesho, msaada huu utasaidia katika kuimarisha
kitengo cha kuhudumia watoto wachanga wanaozaliwa chini ya siku 28 (NICU),"
amesema Dkt. Lulu.
Kwa upande wake Mratibu wa Uboreshaji Endelevu wa Huduma za
Afya kupitia mpango wa NEST360 unaotekelezwa na Taasisi ya Afya Ifakara (IHI)
Dkt. Robert Tillya, amesema kuwa wataendelea kutoa msaada kadri
itakavyowezekana ili kuendelea kuunga mkono juhudi za hospitali za kuboresha
huduma na kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Naye. Daktari Bingwa wa Watoto MNH-Mloganzila ameeleza kuwa asilimi 80 ya watoto wanaozaliwa chini va siku 28 wanapata manjano hivyo mashine hizo zitaongeza idadi ya mashine na kuwezesha watoto wengi kuhudumia kwa wakati mmoja.
0 Maoni