Mloganzila kutibu magojwa ya ngozi na kuondoa tattoo kwa kutumia laser

 

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imekuwa hospitali ya kwanza ya Umma nchini kuanzisha huduma mpya ya kutibu magonjwa ya ngozi kwa kutumia teknolojia mpya na ya kisasa ya mwanga (Laser).

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji MNH-Mloganzila, Dkt. Julieth Magandi alipokuwa kizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanzishwa rasmi kwa huduma hiyo iliyoanza kutolewa rasmi Muhimbili Mloganzila .

“Tunawashukuru wenzetu wa Korea Kusini kwa kutusaidia kuwapatia mafunzo ya namna ya kutumia tiba mwanga kutibu magonjwa mbalimbali ya ngozi, sasa wataalam wetu wana uwezo wa kutosha kutoa huduma hizi,” ameongeza Dkt. Magandi.

Dkt. Magandi ameongeza kuwa hospitali ina wataalam waliobobea katika magonjwa ya ngozi sambasamba na vifaa tiba vya kisasa ambavyo vinapatikana MNH Mloganzila kitu ambacho kinafanya huduma hii kufanyika kwa ufanisi.

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ngozi Dkt. Andrew Foi amesema huduma hii inaweza kusaidia kutibu magonjwa ya ngozi yaliyoshindikana kwenye matibabu ya kawaida na kuboresha muonekano wa ngozi.

Dkt. Foi amesema huduma ya tiba mwanga inahusisha kutibu magonjwa ya ngozi ikiwemo vitiligo, pumu ya  ngozi, saratani ya ngozi, kuondoa tatoo, viotea, michirizi katika sehemu mbalimbali za mwili na nywele ikiwemo usoni (Phototherapy).

Chapisha Maoni

0 Maoni