Serikali imefafanua kuwa itaendelea kuzingatia utoaji wa haki zote kwa wananchi
wanaoamua kwa hiari kuhama kutoka kwenye Hifadhi ya Ngorongoro kupisha uhifadhi
na kwenda kwenye maeneo wanayoyataka ikiwa ni pamoja na maeneo yaliyotengwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya
Ngorongoro Murtalla Mbillu ametoa kauli
hiyo alfajiri ya leo Aprili 7, 2024 Makao
Makuu ya zamani ya Hifadhi ya Ngorongoro
wakati alipokuwa akiwaaga jumla ya wananchi 422
kwenye walioamua kuondoka kwa
hiari kwenye Hifadhi ya Ngorongoro kupisha uhifadhi na kwenda kwenye maeneo waliyoyachagua.
“Bila shaka mnatambua
kuwa pamoja na Serikali kuwalipa fidia
na motisha bado mkifika katika
Kijiji cha Msomera mtapata huduma zote za msingi ikiwa ni pamoja na kupatiwa
nyumba kwenye kiwanja cha ukubwa wa ekari 2.5 na ekari tano za kufanya shughuli za kilimo, eneo la malisho pamoja na
huduma za elimu,afya, umeme na maji,” amesisitiza Mbillu.
Amefafanua kuwa zoezi
la kuhama ni zoezi la hiari
ambapo mtu mwenyewe bila
kushinikizwa na mtu ana hiari ya
kuondoka lakini asitokee mtu wa kuwarubuni na kuwadanganya watu walioamua kuhama
kwa hiari yao kwa kuwa kwa
kufanya hivyo watakuwa wanafanya jinai na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Mwakilishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Msemaji wa
Wizara hiyo, John Mapepele amewapongeza wananchi walioamua kwa
hiari kuondoka kupisha uhifadhi huku akimshukuru rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania. Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake makubwa na dhamira ya
kuboresha maisha ya wananchi.
Aidha, amesema dhamira ya Serikali ni kutaka wananchi wake
wanapata haki zao za msingi za kuishi maisha bora na kupata huduma zote za
kijamii kama elimu na afya bila kubughudhiwa na mtu.
Kaimu Kamishina wa Hifadhi ya Ngorongoro Victoria Shayo
amewataka wananchi hao walioamua kuhama kwa hiari kuwa mabalozi wazuri
kuwashawishi wananchi walibaki kuchukua maamuzi sahihi ya kupisha uhifadhi.
Akitoa taarifa ya zoezi hilo Kaimu Meneja wa Mradi kuhamisha wananchi wa Hifadhi ya
Ngorongoro, Flora Assey kaya 60 zenye watu 353 zimeelekea Kijiji cha Msomera
wakati kaya 13 zenye watu 69 zimeelekea
Meatu Simiyu na kaya zilizobaki zimeelekea simanjiro na Arusha.
0 Maoni