Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi amepokea salamu za
pole kutokana na kifo cha Rais Mstaafu
wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mzee Ali Hassan Mwinyi kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Somalia Mhe.Dkt.Hassan Sheikh
Mohamud.
Viongozi hao walikutana leo tarehe 28 Aprili 2024 Ikulu,
Migombani.
Mzee Mwinyi alifariki dunia tarehe 29 Februari, 2024 Dar es
Salaam na kuzikwa tarehe 02 Machi 2024
kijijini kwake Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Rais Dk.Mwinyi amemshukuru Rais Dkt. Mohamud kwa salamu za mkono wa pole na kuja kuwafariji.
0 Maoni