Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) litafanya Mkutano wa 13 wa
Mwaka wa Kitaaluma kwa siku mbili kuanzia kesho tarehe 29/04/2024 Jijini
Dodoma.
Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dodoma Mjumbe wa
Kamati ya Utendaji TEF, Neville Meena amesema mkutano huo unatarajiwa
kufunguliwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko.
Kauli mbiu ya Mkutano wa 13 wa Mwaka wa Kitaalum wa TEF ni “Uandishi wa habari kuhamasisha matumizi ya gesi kulinda misitu”.
0 Maoni