Wanawake waalikwa Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia

 

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amewaalika wanawake kushiriki katika Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia linalotarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Machi 9 Jijini Dodoma.

Kapinga amesema kuwa kongamano hilo linatarajiwa kuwakutanisha wanawake zaidi ya 4000 kutoka Wilaya na Mikoa mbalimbali ambapo pamoja na mambo mengine wanawake hao watapata fursa ya kujifunza kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha nishati safi inapatikana kwa kila Mtanzania.

Amesema pia Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa nishati safi ya kupikia wanatarajiwa kugawa majiko ya gesi pamoja na majiko banifu ikiwa ni muendelezo wa juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha ifikapo mwaka 2033 zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Chapisha Maoni

0 Maoni