Watu wanane wa familia sita tofauti wamefariki dunia na
wengine 34 wanapatiwa matibabu Hospitali Kisiwa Panza, Mkoa wa kusini Pemba
Visiwani Zanzibar baada ya kula samaki aina ya kasa.
Taarifa kutoka Pemba zinasema kwamba watu hao baada ya kula samaki
huyo aina ya kasa hapo jana walianza kuumwa tumbo, kulegea mwili, kutapika na
kuharisha.
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mattar Zahor, amesema sampuli
za matabishia na damu zimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kutambua
kilichosababisha vifo hivyo.
0 Maoni