Kamanda Mkuu wa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali
Mwinyi amevipongeza Vikosi vya Jeshi la Kujenga Uchumi(JKU), Zimamoto na Uokozi
na Chuo cha Mafunzo kwa ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi
wa madarasa, masoko na vituo vya wajasiriamali.
Rais Dk. Mwinyi amesema hayo akizungumza na Maafisa na
Wapiganaji alipowatembelea Vikosi vya Zimamoto na Uokozi, JKU na Chuo cha
Mafunzo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea Vikosi vya SMZ tarehe:
9 Machi 2024.
Aidha, Rais Dk.Mwinyi amehimiza umuhimu wa nidhamu, uzalendo,
uadilifu na umoja kwa Maafisa na Wapiganaji hao.
Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuboresha
miundombinu ya vikosi hivyo.
0 Maoni