Katika kuhakikisha anafuatilia kwa karibu kero mbalimbali za wananchi
zikiwemo za elimu Mbunge Viti Maalumu katika Mkoa wa Mara, Mhe. Esther Matiko, amekuwa akizitembelea shule kadhaa kujionea
mwenyewe kero mbalimbali.
Safari hii Mhe. Matiko amefika Shule ya Sekondari Tagota
inayopatikana Halmashauri ya Mji wa Tarime na kuzungumza na walimu na wanafunzi
wa shule hiyo, ili kusikia na kujionea kero zinazowakabili.
Huu ni mwendelezo wa Mhe. Matiko katika mpango wake wa ukusanyaji wa
changamoto mbalimbali za kielimu kwenye mkoa huo katika kuelekea Bunge la
Bajeti linalotarajiwa kuaanza vikao vyake mwezi wa nne 2024.
0 Maoni