Waziri Mkuu Majaliwa azindua Kanzidata ya TATO

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na  Naibu Waziri Uchukuzi, David Kihenzile  (kulia) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA), Elias Lukumay  kuingia kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana  jijini Dar es Salaam ambapo Waziri Mkuu alizindua kanzidata  ya TATOA  Disemba 14, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza kabla ya kuzindua  kanzidata  ya madereva wa Chama cha  Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA) kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam, Disemba  14, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).  

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania  (TATOA), Elias Lukumay, hundi ya Shilingi milioni 100 kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea Katesh Wilayani Hanang. Makabidhiano hayo yalifanyika baada ya Waziri Mkuu, kuzindua  kanzidata  ya  Madereva wa TATOA  kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam Diusemba 14, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akiagana na Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania  (TATOA), Elias Lukumay baada ya kuzindua Kanzidata ya  ya TATOA kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam, Disemba 14, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Chapisha Maoni

0 Maoni