Ukraine yasherehekea Krismasi Desemba 25 kwa mara ya kwanza

 

Wakristo wa Ukraine wa Orthodox wanasherehekea kwa mara ya kwanza Sikukuu ya Krismasi Desemba 25 katika mwaka huu.

Kwa utamaduni, Ukraine ilikuwa ikiitumia kalenda ya Julian ambayo pia hutumika nchini Urusi, ambayo siku ya Krismasi huwa ni Januari 7.

Katika kuonyesha kuachana na Urusi, sasa Ukraine imeaamua kuadhimisha Krismasi na mataifa ya magharibi kwa kutumia kalenda ya Gregorian inayotumika katika maisha ya kila siku.

Mwezi Julai, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alibadilisha sheria, na kuwafanya wananchi wa Ukraine kuachana na tamaduni za Urusi za kusherehekea Krismasi Januari.



Chapisha Maoni

0 Maoni