Naibu Waziri Pinda achangia ujenzi wa nyumba za mapadri

 

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda amesheherekea Sikukuu ya Krismasi akiwa katika jimbo lake la Kavuu lililopo wilaya ya Mlele mkoani Katavi.

Akiwa jomboni humo, Naibu Waziri Pinda alishiriki  ibada ya Krismasi katika Kanisa Katoliki Parokia Teule ya Bikira Malia Mpalizwa Mbinguni Kibaoni ambako alishiriki pia harambee ya ya ujenzi wa nyumba za mapadri wa kanisa hilo na kuahidi  kuchangia mifuko 200 ya Saruji. Ujenzi wa nyumba hizo utagharimu shilingi milioni 75.

Ibada hiyo ya Krismasi katika kanisa hilo ilihudhuriwa pia na kaka yake Mhe. Pinda ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Kayanza Peter Pinda.

Aidha, Naibu Waziri Pinda akiwa eneo la Kibaoni ambapo ndipo yalipo makazi yake wilayani Mlele mkoani Katavi alijumuika na baadhi ya  wananchi wa eneo hilo wakiwemo viongozi wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mlele katika kusheherekea siku hiyo ya Noeli. 

Naibu Waziri Pinda yuko jimboni kwake katika jimbo la Kavuu wilayani Mlele mkoa wa Katavi pamoja na mambo mengine kujumuika  na wapiga kura wake kutafakari utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika jimbo hilo.

Na. Munir Shemweta- WANMM Mlele

Chapisha Maoni

0 Maoni