WHO yasema hospitali ya Al-Shifa yageuka eneo la makaburi

 

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kwamba hospitali kubwa ya Gaza ya Al-Shifa inakaribia kuwa “eneo la makaburi” kutokana na miili ya watu kujaa ndani na nje.

Makumi ya watoto njiti na wagonjwa 45 wa figo wanaohitaji kufanyiwa dialysis hawawezi kutibiwa kwa usahihi kutokana na kukosekana kwa umeme, Msemaji wa UN amesema.

Mapigano yamekuwa yakishamiri karibu na hospitali kwenye Jiji la Gaza katika siku za hivi karibuni, huku uhaba mkubwa wa mafuta ukiathiri matibabu.

Israel imekuwa ikiwatuhumu Hamas kwa kutumia hospitali kuanzisha mashambulizi yao, huku hospitali hiyo na Hamas wakikanusha madai hayo.

Israel ilianza kushambulia Gaza, baada ya Hamas kufanya shambulizi Oktoba 7, ambalo liliua watu 1,200 na zaidi ya 200 wakipelekwa hospitali.

Chapisha Maoni

0 Maoni