Waziri wa Nchi Ofisi Rais
TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema serikali itawalipa wakazi wa Bonde la Mto
Msimbazi kuanzia leo Novemba 16, 2023 ambapo hadi sasa asilimia zaidi ya 92
wameshahakikiwa na wanasubiri kulipwa.
Mhe. Mchengerwa amefafanua
kuwa fidia itakayolipwa ni ya uthamini wa jengo na sio Ardhi, kwa mujibu wa
sheria hawapaswi kulipwa fidia ya Ardhi kwa sababu wakazi hao wamejenga katika
maeneo hatarishi lakini kwa upendo wa kipekee wa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu
Hassan ameelekeza kila mkazi wa eneo hilo atapewa kifuta jasho cha shilingi
milioni 4 kiasi ambacho kiko nje ya fidia halisi ya Jengo.
Aidha, Waziri wa OR-TAMISENI
amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu amedhamiria
kufanya Ujenzi wa kisasa wa barabara ya juu Jangwani ambayo inakwenda kuondoa
kero ya mafuriko hivyo Ujenzi huo unakwenda sambamba na maboresho na
uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi kwa ujumla wake.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan
kwa uwekezaji mkubwa anaoufanya katika Mkoa huo wenye masilahi mapana ya Umma
ambapo amewataka wananchi na wakazi wa Bonde la Mto Msimbazi kutii Kauli ya
Serikali kamywe wasirubuniwe wala kudanganyana Serikali inafanya uwekezaji
Msimbazi kwa masilahi mapana ya watu wengi " Mtu anakudanganya usisaini
kuchukua fidia hiyo wakati yeye alishasini siku nyingi, mkitaka niwataje
nitawataja".
0 Maoni