Mchengerwa aridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa soko la Kariakoo

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe Mohamed Mchengerwa akiwa ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ametembelea na kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Soko la Kisasa la Kariakoo ambapo amesema ameridhishwa na maendeleo ya Ujenzi huo.

Amemshukuru Mhe Rais Dkt Samia kwa kutoa pesa ambazo zinawezesha utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kisasa ambao kukamilika kwake utafungua fursa nyingi pamoja na kuchukua wafanyabishara wengi zaidi tofauti na ilivyokua awali.

Aidha, Mhe. Mchengerwa amemtaka mkandarasi kuendelea kujenga katika kiwango stahiki, kuzingatia ubora na thamani ya pesa, pia amesema Soko likikamilika atamuomba Mhe Rais aje kulifungua rasmi.

Vilevile Mhe Albert Chalamila amemshukuru Rais Dkt Samia na Waziri wa OR-TAMISENI ambapo amesema amepokea maelekezo yake yatafanyiwa kazi kwa wakati, pia amemhakikishia kuendelea kumlipa mkandarasi pesa kwa wakati hata hivyo ametoa tahadhari kwa wananchi kuepuka matapeli hadi sasa hakuna chumba kilichopangishwa muda ukifika utaratibu utakuwa wazi lakini kikubwa wananchi wajue uwekezaji uliofanyika ni mkubwa hivyo hata Kodi zitapitiwa tena ili ziendane na uhalisia.

Hata hivyo amewataka watakao pata fursa ya kufanya biashara katika Soko hilo kulipa Kodi na sio kukwepa kodi, amesistiza kwa kutambua umuhimu wa Kariakoo Serikali inaendelea Kuimarisha Ulinzi na Usalama ili watu wafanye biashara saa 24 pia mifumo ya CCTV camera itafungwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni