Filamu ya The Royal Tour
iliyochezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan imezaa Epic Tanzania Tour.
Ziara hii ya awali ya EPIC
ina wawekezaji 180 kutoka Marekani wanaotembelea Serengeti na Ngorongoro ambapo
ziara pili itafanyika mwanzoni mwa Desemba na itajumuisha magwiji wa tennis
duniani ambao watatoana jasho katikati ya Hifadhi ya Serengeti.
Miongoni mwa watopezi wa
mchezo wa Tennis wanaotarajiwa kuwasili nchini ni Gigi Fernandez, John McEnroe
pamoja na Mac Roy.
Program ya EPIC Tanzania
Tour inaratibiwa na Kampuni ya Goshen Safari kwa kushirikiana na Serikali
ambapo kundi hili linatarajiwa kuagwa rasmi na Serikali baada ya kuhitimisha
ziara yake Novemba 12, 2023 ambapo Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe, Angellah
Kairuki atatoa kauli ya Serikali.
Picha na habari na John Mapepele
0 Maoni