Rais wa Romania, Mheshimiwa
Klaus Iohannis, amewasili nchini kwa ziara ya Kitaifa kuanzia leo tarehe 16
hadi 19 Novemba 2023 kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Alipowasili katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere amepokelewa na Waziri wa Maliasili na
Utalii Mhe. Angellah Kairuki.
Lengo la ziara hiyo ni
pamoja na kushawishi uwekezaji zaidi na kuvutia watalii wengi kutoka nchini
Romania.
Aidha katika mazungumzo
rasmi yatakayofanyika tarehe 17 Novemba 2023 Rais huyo na mwenyeji wake
watajadili namna bora ya kukuza na kuimarisha ushirikiano kati sekta za elimu,
afya, kilimo nishati na madini.
Kabla ya kuondoka nchini
tarehe 19 Novemba 2023 Rais wa Romania atapata fursa ya kwenda Zanzibar ambapo
atazungumza na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi na kutembelea mji mkongwe ambao ni
moja kati ya vivutio vikubwa vya utalii duniani.
0 Maoni