Rais wa Kenya apiga marufuku uagizaji mahindi kutoka nje

 

Rais William Ruto wa Kenya amepiga marufuku kuingiza mazao ya nafaka ya mahindi na ngano kutoka nje ya nchi ili kulinda soko la ndani dhidi ya mazao yanayoingizwa nchini humo na kuuzwa bei nafuu hali inayoathiri bei za nafaka.

Rais Ruto amesitisha utoaji vibali vipya vya kuagiza nafaka kutoka nje ya nchi, na kusema kwamba Serikali yake itabadili msimamo wake huo pale tu itakapobainika nchi inakabiliwa na uhaba wa nafaka.

Pia, amebainisha kwamba Serikali ya Kenya imetenga shilingi bilioni 4 za nchi hiyo kwa ajili ya kununua mahindi kutoka kwa wakulima ambao wameshaanza kuvuna mazao yao, kabla ya kuanza mvua za El Nino.

Agizo hilo la Ruto, litaziathiri baadhi ya nchi za Afrika Mashariki ambazo zimekuwa zikiiuzia Kenya mazao ya nafaka hususan mahindi, ambapo Tanzania na Uganda ni mingoni mwa nchi ambazo hunufaika na soko la mazao la Kenya.

CHANZO: Nation

Chapisha Maoni

0 Maoni