Mamlaka za afya nchini Algeria, zimeimarisha hatua za
kudhibiti mipaka kuzuia kusambaa kwa kunguni, ambao wametapakaa nchi ya Ufaransa.
Wizara ya Afya ya Taifa hilo la Kaskazini mwa Afrika,
imesema imekuwa ikichukua hatua za kunyunyizia dawa za kulia wadudu kwenye
ndege, meli na magari yanayoingia nchini humo.
Hatua hizo zinakuja baada ya wadudu hao wanafyonza damu kuwa
na uwezekano wa kuingia Algeria kutokana na idadi kubwa ya watu wanaosafiri
kutoka Ufaransa.
Hata hivyo wizara hiyo imesema, hakuna kunguni waliongia
Algeria kutoka Ufaransa, na kuhimiza wananchi kuendelea kuchukua tahadhari.
Nchi ya jirani ya Morocco nayo tayari imeshatangaza hatua za
kuzuia hatari ya kuingia kunguni hao kutoka Ufaransa.
0 Maoni