Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo
Oktoba 5, 2023 ametembelea Hospitali ya Aga Khan - Tanzania kujionea namna
hospitali hiyo inavyotoa huduma za afya kwa jamii, ikitumia vifaa tiba vya
teknolojia ya kisasa.
RC Chalamila akiwa Hospitalini hapo ametembelea maeneo
mbalimbali yenye vifaa tiba vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu
ya utoaji huduma za Afya pia amejionea Ujenzi wa jengo maalum litakalo toa
huduma za kutibu magonjwa ya Cansa.
Vilevile Mhe Albert Chalamila amepongeza kazi nzurii
inayofanywa ya kupambana na adui maradhi ambayo inamatokeo ya moja kwa moja
kwenye kukuza na kuimarisha uchumi na maendeleo ya nchi ambayo ndiyo dhamira ya
Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Watanzania, pia amefurahishwa na miundo mbinu
ya hospitali hiyo, wataalam wenye uwezo mkubwa, usafi wa mandhari na mapangilio
wa vitu.
Aidha, Mkuu wa Mkoa ameutaka uongozi wa hospitali hiyo kuwa
uhuishaji wa taaluma za watumishi iwe ni tabia isiyo na kikomo, vilevile
kusimamia vizuri upatikanaji wa huduma kwa gharama ambayo watu wengi wanaweza
kumudu.
Kwa upande wa Mtendaji Mkuu wa hospitali ya Aga Khan Dar es
Salaam Tanzania Sisawo Konteh amesema wamekua wakipata ushirikiano mkubwa
kutoka serikarini na amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa Aga Khan itaendelea kuwekeza
Dar es Salaam kwa masilahi mapana ya Umma.
Mwisho Mhe Albert Chalamila katika ziara yake ameambatana na
Katibu Tawala wa Mkoa Bi Rehema Madenge, wataalam kutoka Idara ya Afya, DAWASA,
TANESCO, na TRA.
0 Maoni