Msako wa kitaifa umeanzishwa kumtafuta mtuhumiwa wa makossa
ya ugaidi aliyewahi kuwa mwanajeshi, ambaye ametoroka gerezani Jumatano
asubuhi.
Mtuhumiwa huyo Daniel Abed Khalife, 21, alikuwa anangojea kusikilizwa
kesi zake HMP Wandsworth, Jijini London baada ya kutuhumiwa kuacha mabomu
feki kwenye kambi ya jeshi.
Inaaminika kwamba mfungwa huyo alitoroka kupitia jiko la
gereza kwa kujificha chini ya gari la kusambaza vyakula.
Ulinzi wa ziada umeimarishwa kwenye viwanja vya ndege na
kwenye bandari na kusababisha kuchelewesha usafiri kwa muda mrefu.
0 Maoni