Prof. Ndalichako ahimiza ushirikiano kuwahudumia wananchi

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amewataka watendaji wake kushirikiana kwa pamoja ili wananchi wapate huduma kwa wakati.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo wakati wa kikao kazi cha kujadili kazi za Ofisi hiyo pamoja na Taasisi zilizopo chini yake kilichofanyika Septemba 6, 2023 katika jengo la OSHA jijini Dodoma.

Aidha Prof. Ndalichako ameongeza kuwa kila mtendaji anajukumu la kutekeleza maagizo ya viongozi kwa haraka ili kuiwezesha serikali kufikia malengo na kuleta tija kwa wananchi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu- Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhandisi Cyprian Luhemeja amemuhakikishia Waziri Ndalichako kuwa majukumu ya ofisi hiyo yatatekelezwa kwa kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. John Mduma akiongea kwa niaba ya Wakurugenzi Watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo, amebainisha kuwa wataendelea kutoa ushirikiano kwa Katibu Mkuu huyo mpya ili kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya wizara pamoja na taasisi zake.

Chapisha Maoni

0 Maoni