Jaribio la mapinduzi ya kijeshi lazimwa nchini Burkina Faso

 

Idara ya Usalama na Intelejensia ya Burkina Faso imezima jaribio la mapinduzi Jumanne, kwa mujibu wa Serikali ya kijeshi ya nchi hiyo.

Imedaiwa kuwa baadhi ya maafisa wa jeshi na watu wengine walipanga kutibua hali ya usalama wa nchi hiyo na kuitumbukiza kwenye machafuko.

Tukio hilo limetokea ikiwa ni chini ya mwaka mmoja, tangu rais wa mpito wa nchi hiyo Kapteni Ibrahim Traore atwae madaraka kwa njia ya mapinduzi.

Taarifa iliyosomwa kupitia televisheni, imeeleza mamlaka ya Burkina Faso imewakamata baadhi ya wahusikawa jaribio la mapinduzi, bila ya kutoa taarifa zaidi.

Chapisha Maoni

0 Maoni