Rais Dk. Mwinyi asema Zanzibar kuwa kivutio cha kijani na utalii endelevu

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali inatambua fursa zilizopo katika Kilimo Hai kupitia mkakati uliondaliwa na Wizara ya kilimo kwa kushirikiana na wadau utakuwa ni suluhisho kwa changamoto za sekta ya Kilimo Hai ikiwemo upatikanaji wa pembejeo za kibaolojia, elimu kwa wakulima na wafugaji pamoja na upatikanaji wa masoko ya ndani na nje ya nchi ya bidhaa zinatokana na Kilimo Hai.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo jana wakati akifungua Tamasha la Kilimo Hai na kutembelea mabanda ya maonesho katika viwanja vya Dole Kizimbani, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameeleza matumaini yake kupitia mkakati uliondaliwa na Serikali kuwa utatengeneza programu madhubuti ya utekelezaji ya kuwapa fursa vijana kwa kuanzisha biashara za kutengeneza viatilifu na mbolea hai ili kusaidia upatikanaji wa masoko ya ndani na nje ya nchi na kuitangaza Zanzibar kuwa kivutio cha kijani na kuendana na utalii endelevu.

Halikadhalika Rais Dk. Mwinyi ametoa wito katika utoaji wa elimu kwa watumiaji na walaji kuzifahamu faida za Kilimo Hai kuepusha chakula kinachozalishwa kupitia matumizi ya kemikali ili kupunguza maradhi yasiyoyambukiza ikiwemo saratani, shinikizo la damu na kisukari.

Chapisha Maoni

0 Maoni