Rais Samia abadilishana mawazo na Rais Lula wa Brazil

 

Rais Samia Suluhu Hassan akibadilishana mawazo na Rais wa Brazil, Lula Da Silva pamoja na Waziri wa mambo ya nje wa Urusi muda huu baada ya kukamilika kwa mkutano wa kumi na tano wa Jumuiya ya BRICS.

BRICS ni Jumuiya kubwa ya pili kiuchumi duniani, ikiwakilisha idadi ya watu wanaokaribia bilioni 3.5 inaundwa na nchi za Urusi, China, Brazil, Afrika ya Kusini na India.

Saudi Arabia, Egypt, UAE, Argentina, Iran na Ethiopia watakuwa ni wanachama wapya kuanzia january Mosi, 2024

Asilimia 80 ya uzalishaji wa mafuta unatoka katika nchi zinazounda umoja wa BRICS.

Chapisha Maoni

0 Maoni