Mmiliki wa gari iliyoua mwanafunzi aangua kilio mahakamani

 

Malima Masota anayedaiwa kuendesha gari kwa mwendo kasi na kusababisha kifo cha mwanafunzi Consolatha Marwa ameangua kilio mahakamani baada ya kukosa dhamana kwa kushindwa kutimiza masharti.

Dereva huyo amesomewa mashtaka yanayomkabili likiwemo la kuendesha gari kwa kwendo kasi na kusababisha kifo cha mwanafunzi huyo aitwaye Consolatha kinyume na kifungu namba 40, 63 (2) (a) naa 26 (1) (a)cha sheria ya usalama barabarani namba 168 marejeo ya mwaka 2002 na kumjeruhi mwanafunzi mwingine aitwaye Magreth Ntemi pamoja na kuendwsha gari isiyokuwa na bima kinyume na kifungu namba 4(1) na 2 cha sheria ya bima ya magari namba 169 marejeo 2002.

Mmiliki wa gari hilo lenye namba za usajili T. 121 DCU, Athuman Mussa ameangua kilio katika mahakama ya wilaya ya Magu baada ya kushindwa kutumiza masharti ya dhamana ambapo dereva na mmliki wa gari hilo walifunguliwa kesi ya trafiki namba 19 ya mwaka huu ambayo imesomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Amon Rwegoshora

Baada ya kusomewa mashtaka mshtakiwa namba moja, amekidhi masharti ya dhamana ambayo ni kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika watakaosaini bondi ya maneno ya sh milioni 4 kila mmoja huku mshtakiwa namba mbili akishindwa kukidhi masharti hayo kutokana na kuwa na mdhamini mmoja na kurudishwa rumande katika gereza la wilaya ya Magu.

Mwendesha Mashtaka, Ilole amesema upelelezi wa kesi hiyo umekamilika, huku Hakimu, Rwegoshora akiahirisha kesi hiyo hadi Agosti 31, mwaka huu itakapotajwa kwa ajili ya washtakiwa kuanza kusomewa maelezo ya awali.

Ajali hiyo ilitokea Agosti 11, 2023 majira ya saa saba mchana katika mtaa wa Nyalikungu "A" wilayani Magu mkoa wa Mwanza iliyohusisha gari yenye namba za usajili T.121 DCU aina ya Toyota Hiace ambapo dereva wa gari hiyo alitoroka baada ya ajali na baadae kukamatwa na jeshi la polisi.

Kupitia taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari Agosti 12 mwaka huu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza SACP Wilbrod Mutafungwa alisema ajali hiyo iliyotokea katika mtaa wa Nyalikungu 'A' wilayani Magu, kwa gari hilo kuwagonga wanafunzi waliokuwa wakivuka barabara na kusababisha kifo cha mwanafunzi mmoja na kujeruhi mwingine.

Chapisha Maoni

0 Maoni